Hamia kwenye habari

Amani Duniani—Itapatikanaje?

Amani Duniani—Itapatikanaje?

Jibu la Biblia

 Amani haitaletwa duniani kupitia jitihada za wanadamu, bali kupitia Ufalme wa Mungu, serikali ya kimbingu inayoongozwa na Kristo Yesu. Ona jinsi Biblia inavyotufundisha kuhusu tumaini hilo zuri ajabu.

  1.   Mungu ‘atakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia,’ na hivyo kutimiza ahadi yake ya kuleta “amani duniani kwa watu anaowafadhili!”—Zaburi 46:9; Luka 2:14, Biblia Habari Njema.

  2.   Ufalme wa Mungu ukiwa mbinguni utaitawala dunia yote. (Danieli 7:14) Utakapoitawala dunia, Ufalme huo utaondoa utaifa, ambao ni chanzo kikuu cha mizozo mingi.

  3.   Yesu, Mtawala wa Ufalme wa Mungu, anaitwa “Mkuu wa Amani,” na atahakikisha kwamba ‘hakutakuwa na mwisho wa amani.’—Isaya 9:6, 7.

  4.   Watu walioazimia kuendelea kupigana hawataruhusiwa kuwa raia wa Ufalme huo, kwa kuwa “mtu yeyote anayependa jeuri nafsi [ya Mungu] hakika inamchukia.”—Zaburi 11:5; Methali 2:22.

  5.   Mungu anawafundisha watu wanaomtii jinsi ya kuishi kwa amani. Ikifafanua matokeo ya elimu hiyo, Biblia inasema: “Watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu. Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”—Isaya 2:3, 4.

 Tayari mamilioni ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wanajifunza kutoka kwa Mungu jinsi ya kuishi kwa amani. (Mathayo 5:9) Ingawa tunatoka katika makabila mbalimbali na tunaishi katika nchi tofauti-tofauti 230, tunakataa kupigana vita na wanadamu wenzetu.

Mashahidi wa Yehova wanajifunza jinsi ya kuishi kwa amani leo