Hamia kwenye habari

MISTARI YA BIBLIA YAFAFANULIWA

Waroma 5:8—“Kristo Alikufa kwa Ajili Yetu, Tulipokuwa Tungali Wenye Dhambi”

Waroma 5:8—“Kristo Alikufa kwa Ajili Yetu, Tulipokuwa Tungali Wenye Dhambi”

 “Mungu hupendekeza upendo wake kwetu kwa kuwa tulipokuwa bado watenda dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.”—Waroma 5:8. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

 “Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.”—Warumi 5:8. Union Version

Maana ya Waroma 5:8

 Yehova a Mungu alionyesha upendo mwingi alipomruhusu Mwana wake, Yesu Kristo afe kwa ajili ya wanadamu wenye dhambi. (Yohana 3:16) Kwa kuwa wanadamu ni watenda dhambi, wana mwelekeo wa kufikiri na kutenda kwa njia inayokiuka viwango vya uadilifu vya Mungu. (Wakolosai 1:21, 22) Hata hivyo, Mungu alifanya iwezekane kwetu kupatanishwa tena naye “kupitia kifo cha Mwana wake.” (Waroma 5:10) Kwa sababu hiyo, tuna nafasi ya kuwa na uhusiano mzuri na Mungu sasa na tarajio la kupata uzima wa milele wakati ujao.—Waroma 5:11; 1 Yohana 4:9, 10.

Muktadha wa Waroma 5:8

 Mtume Paulo aliwaandikia Wakristo walioishi Roma maneno hayo. Katika sura ya 5 ya barua yake kwa Waroma, Paulo alieleza kwa nini Wakristo wangeweza kushangilia na kuwa na uhakika katika tumaini lao. (Waroma 5:1, 2) Tumaini hilo “halikatishi tamaa,” kwa sababu linategemea upendo mwingi ambao Mungu ameonyesha kupitia Yesu. (Waroma 5:5, 6) Yesu alidumisha utii mkamilifu kwa Mungu, jambo ambalo mwanadamu wa kwanza, Adamu alishindwa kufanya. (Waroma 5:19) Kwa sababu ya kutotii, Adamu aliwapitishia wazao wake dhambi na kifo. (Waroma 5:12) Tofauti na Adamu, utii mkamilifu wa Yesu na kifo chake cha kidhabihu kilifanya iwezekane kwa wanadamu watiifu kuwa na tumaini la kuishi milele.—Waroma 5:21.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.—Zaburi 83:18.