Methali 18:1-24

  • Kujitenga na wengine ni jambo la kichoyo lisilo la hekima (1)

  • Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu (10)

  • Mali ni ulinzi wa kuwaziwa tu (11)

  • Hekima ya kusikiliza pande zote mbili (17)

  • Rafiki hushikamana na mtu kwa ukaribu kuliko ndugu (24)

18  Yeyote anayejitenga na wengine anafuatia tamaa zake mwenyewe za kichoyo;Hukataa* hekima yote inayotumika.   Mtu mpumbavu hapendezwi na uelewaji;Anaona ni afadhali afunue yaliyo moyoni mwake.+   Mtu mwovu anapokuja, dharau huja pia,Na aibu huja pamoja na fedheha.+   Maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina.+ Chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.   Si vema kumpendelea mwovu+Wala kumnyima haki mtu mwadilifu.+   Maneno ya mpumbavu husababisha ugomvi,+Na kinywa chake hualika kipigo.+   Kinywa cha mpumbavu ndicho kinachomwangamiza,+Na midomo yake ni mtego kwa uhai wake.*   Maneno ya mchongezi ni kama matonge matamu;*+Humezwa na kushuka tumboni moja kwa moja.+   Yeyote aliye mvivu katika kazi yakeNi ndugu ya mtu mharibifu.+ 10  Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu.+ Mwadilifu hukimbilia humo na kupata ulinzi.*+ 11  Mali ya tajiri ni jiji lake lenye ngome;Ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+ 12  Kabla ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mtu huwa na kiburi,+Na kabla ya utukufu kuna unyenyekevu.+ 13  Yeyote anayejibu kabla ya kusikia ukweli wa mambo,Huo ni upumbavu na aibu kwake.+ 14  Roho ya mtu inaweza kumtegemeza anapokuwa mgonjwa,+Lakini ni nani anayeweza kustahimili roho iliyopondeka?*+ 15  Moyo wa mtu mwenye uelewaji hupata ujuzi,+Na sikio la mwenye hekima hujitahidi kupata ujuzi. 16  Zawadi ya mwanadamu humfungulia njia;+Humwezesha kufika mbele ya watu mashuhuri. 17  Mtu wa kwanza kuwasilisha kesi yake huonekana kuwa sahihi,+Mpaka mwingine anapokuja na kumuuliza maswali.*+ 18  Kupiga kura hukomesha mizozo+Na kukata maneno kati ya* wapinzani wenye nguvu. 19  Ndugu aliyekosewa ni mgumu kuliko jiji lenye ngome,+Na kuna mizozo ambayo ni kama makomeo ya ngome.+ 20  Tumbo la mtu litajazwa matunda ya maneno yake;*+Atashiba mazao ya midomo yake. 21  Kifo na uhai viko katika nguvu za ulimi;+Wale wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.+ 22  Anayepata mke mwema amepata kitu chema,+Naye hupata kibali cha* Yehova.+ 23  Maskini husihi anapoongea,Lakini tajiri hujibu kwa ukali. 24  Kuna marafiki walio tayari kuangamizana,+Lakini kuna rafiki anayeshikamana na mtu kwa ukaribu kuliko ndugu.+

Maelezo ya Chini

Au “Hudharau.”
Au “nafsi yake.”
Au “vitu vinavyomezwa kwa pupa.”
Tnn., “na kuinuliwa juu,” yaani, hawezi kufikiwa, yuko salama.
Au “iliyokata tamaa kabisa?”
Au “kumhoji.”
Tnn., “Na kuwatenganisha.”
Tnn., “kinywa chake.”
Au “nia njema ya.”