Methali 19:1-29

  • Ufahamu hutuliza hasira (11)

  • Mke mgomvi ni kama paa linalovuja (13)

  • Mke mwenye busara hutoka kwa Yehova (14)

  • Mtie mtoto nidhamu wakati bado kuna tumaini (18)

  • Hekima ya kusikiliza mashauri (20)

19  Ni afadhali kuwa maskini na kutembea kwa utimilifu+Kuliko kuwa mpumbavu na kusema uwongo.+   Mtu asiye na ujuzi si mtu mzuri,+Na mtu anayetenda bila kufikiri* anatenda dhambi.   Ujinga wa mtu ndio unaopotosha njia yake,Kisha moyo wake unamkasirikia vikali Yehova.   Mali huwavuta marafiki wengi,Lakini maskini ataachwa hata na rafiki yake.+   Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,+Na yule anayesema uwongo kila anapopumua hataponyoka.+   Wengi hujipendekeza kwa mtu maarufu,*Na kila mtu ni rafiki ya yule anayetoa zawadi.   Ndugu wote wa mtu maskini humchukia;+Marafiki zake humwepuka hata zaidi!+ Huwafuatia ili awasihi, lakini hakuna yeyote anayemsikiliza.   Yeyote anayepata busara* anajipenda mwenyewe.*+ Yeyote anayethamini utambuzi kama hazina atapata mafanikio.*+   Shahidi anayesema uwongo hatakosa kuadhibiwa,Na yule anayesema uwongo kila anapopumua ataangamia.+ 10  Mjinga hastahili kuishi maisha ya anasa;Sembuse mtumishi kuwatawala wakuu!+ 11  Ufahamu wa mtu hakika hutuliza hasira yake,+Na ni fahari kwake kuachilia* kosa.+ 12  Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba,*+Lakini kibali chake ni kama umande juu ya majani. 13  Mwana mpumbavu humletea shida baba yake,+Na mke mgomvi* ni kama paa ambalo haliachi kamwe kuvuja.+ 14  Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa akina baba,Lakini mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.+ 15  Uvivu huleta usingizi mzito,Na mtu mzembe atakaa njaa.+ 16  Anayeshika amri anaulinda uhai wake;*+Asiyejali njia zake atakufa.+ 17  Anayemwonyesha kibali mtu wa hali ya chini anamkopesha Yehova,+Naye Atamlipa* kwa anayotenda.+ 18  Mtie nidhamu mtoto* wako wakati bado kuna tumaini,+Nawe usiwajibike kwa* kifo chake.+ 19  Mtu mwenye hasira kali atalipia adhabu;Ukijaribu kumwokoa, utalazimika kufanya hivyo tena na tena.+ 20  Sikiliza mashauri na ukubali nidhamu,+Ili uwe na hekima wakati wako ujao.+ 21  Moyo wa mwanadamu una mipango mingi,Lakini shauri* la Yehova ndilo litakalodumu.+ 22  Kinachomfanya mtu awe mwenye kutamanika ni upendo wake mshikamanifu;+Na ni afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo. 23  Kumwogopa Yehova huongoza kwenye uzima;+Yule aliye na woga huo atakuwa na pumziko jema, hatapatwa na madhara.+ 24  Mvivu huutumbukiza* mkono wake katika bakuli la karamu,Lakini hata hashughuliki kuurudisha kinywani mwake.+ 25  Mpige mwenye dhihaka,+ ili mjinga awe mwerevu,+Mkaripie mwenye uelewaji ili aongeze ujuzi wake.+ 26  Yule anayemtendea vibaya baba yake na kumfukuza mama yakeNi mwana anayeleta aibu na fedheha.+ 27  Mwanangu, ukiacha kusikiliza nidhamu,Utatangatanga mbali na maneno ya ujuzi. 28  Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki haki,+Na kinywa cha waovu hubugia uovu.+ 29  Hukumu inawangojea wadhihaki,+Na mgongo wa wapumbavu unangojea mapigo.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “anayetembea haraka.”
Au “mkarimu.”
Tnn., “mema.”
Au “anaipenda nafsi yake.”
Tnn., “moyo.”
Tnn., “kupita.”
Au “mwanasimba mwenye manyoya marefu shingoni.”
Au “msumbufu.”
Au “anailinda nafsi yake.”
Au “Atamthawabisha.”
Au “mwana.”
Au “usitamani.”
Au “kusudi.”
Tnn., “huuzika.”