Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Mungu Anakujali

Mungu Anakujali

BIBLIA ndio chanzo bora zaidi cha mwongozo wa kiroho, kwa sababu inatoka kwa Mungu. Biblia si kitabu cha afya, lakini inaweza kutusaidia kwa njia inayofaa kushughulikia hali ngumu, kuvurugika kwa mawazo, maumivu ya hisia, na hali mbaya ya afya ya mwili na akili.

Jambo muhimu zaidi ni kwamba Biblia inatuhakikishia kuwa Muumba wetu, Yehova Mungu, a anaelewa mawazo na hisia zetu vizuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote. Anatamani kutusaidia kukabiliana na hali yoyote inayotupata. Kwa mfano, chunguza Maandiko haya mawili yanayofariji:

“Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; huwaokoa waliopondeka roho.”​—ZABURI 34:18.

“Mimi, Yehova Mungu wako, ninaushika kwa nguvu mkono wako wa kulia, Mimi ninayekuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”​—ISAYA 41:13.

Yehova anatusaidiaje kukabiliana na matatizo ya afya ya akili? Kama tutakavyoona katika makala zinazofuata, Yehova anaonyesha anatujali kikweli kupitia njia nyingi.

a Yehova ni jina la kibinafsi la Mungu.​—Zaburi 83:18.