Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kyrgyzstan

MATUKIO MUHIMU YA MWAKA ULIOPITA

Kuwekwa Wakfu kwa Ofisi za Tawi

Kuwekwa Wakfu kwa Ofisi za Tawi

KWA mwaka mmoja na nusu, wajitoleaji wa ujenzi wenyeji na wageni pia walifanya kazi kwa bidii kuboresha na kupanua ofisi ya tawi ya Bishkek, mji mkuu wa Kyrgyzstan. Programu ya wakfu ilifanyika Oktoba 24, 2015, mwezi mmoja tu baada ya mradi huo kukamilika. Zaidi ya wahudhuriaji 3,000 waliokusanyika katika Majumba ya Ufalme 18 na vituo vingine 5 walifurahia kusikiliza programu hiyo kwa kuunganishwa kupitia intaneti. Stephen Lett, mshiriki wa Baraza Linaloongoza alitoa hotuba ya wakfu yenye kuchochea ambayo ilikuwa na kichwa “Mtumikie Yehova kwa Moyo Kamili.” Siku iliyofuata, kulikuwa na programu yenye kuimarisha imani kwa ajili ya wote nchini humo.

Kyrgyzstan branch

Jumamosi, Mei 14, 2016, wahudhuriaji 6,435 walikusanyika kwa ajili ya programu ya kuwekwa wakfu ofisi ya tawi ya Armenia, ambayo ni orofa sita katika jengo maridadi lenye ghorofa 18. Pia, Jumba la Kusanyiko na majengo kwa ajili ya Shule ya Waeneza Injili yaliwekwa wakfu. Hotuba zilieleza jinsi utendaji wa watumishi wa Yehova nchini humo ulivyoanza. Kazi ya Mashahidi ilianzia kwa wahamiaji Waarmenia waliokuwa nchini Marekani mwanzoni mwa karne ya 20, na kisha nchini Armenia katikati ya miaka ya 1970, nchi hiyo ilipokuwa bado sehemu ya Muungano wa Sovieti. Hivi karibuni, shirika la Mashahidi wa Yehova lilisajiliwa kisheria na ofisi ya tawi ikaanzishwa. Wahudhuriaji wengi hawakudhani kwamba nchi yao ingefanya maendeleo hayo makubwa ya kiroho. Programu ilifikia tamati wahudhuriaji wote walipokubaliana na ndugu David Splane, mshiriki wa Baraza Linaloongoza kuweka wakfu kwa Yehova makao hayo maridadi.

Armenia

Juu: Programu ya kuweka wakfu ofisi ya tawi ya Armenia

Katikati: Ndugu na dada waliohudhuria programu ya pekee iliyofanywa mwishoni mwa juma

Chini: Dansi ya kitamaduni ya Armenia iliyochezwa jioni