Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Dini Yao Tu Ndiyo Dini ya Kweli?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Dini Yao Tu Ndiyo Dini ya Kweli?

 Watu ambao wanachukua mambo ya dini kwa uzito wanapaswa kuhakikisha kwamba dini ambayo wamechagua inakubalika mbele za Mungu na Yesu. La sivyo, mbona mtu ajihusishe nayo? Yesu Kristo hakukubaliana na maoni ya kwamba kuna dini nyingi, au barabara nyingi, na eti zote zinaongoza kwenye wokovu. Badala yake alisema: “Lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.” (Mathayo 7:14) Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba wameipata barabara hiyo. La sivyo, wangetafuta dini nyingine.