Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Hutoa Fungu la Kumi?

Je, Mashahidi wa Yehova Hutoa Fungu la Kumi?

 La, Mashahidi wa Yehova hawatoi fungu la kumi; kazi yetu inategemezwa na michango ya hiari. Kutoa fungu la kumi kunamaanisha nini, na kwa nini Mashahidi wa Yehova hawatoi fungu la kumi?

 Amri ya kutoa fungu la kumi, au sehemu ya kumi ya mali ya mtu ilikuwa sehemu ya Sheria ambayo taifa la kale la Israeli lilipewa. Hata hivyo, Biblia inaonyesha wazi kwamba Sheria hiyo​—kutia ndani “amri ya kukusanya sehemu za kumi”​—haiwahusu Wakristo.​—Waebrania 7:5, 18; Wakolosai 2:13, 14.

 Badala ya kutoa fungu la kumi na matoleo, Mashahidi wa Yehova huwaiga Wakristo wa mapema na kutegemeza kazi yao ya kuhubiri katika njia mbili: kwa kuhubiri na kufundisha bila malipo na kwa kutoa michango ya hiari.

 Kwa kufanya hivyo tunaiga mwongozo ambao Biblia inatoa kwa Wakristo: “Kila mmoja na afanye kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.”​—2 Wakorintho 9:7.