Yobu 34:1-37

  • Elihu anatetea haki na njia za Mungu (1-37)

    • Yobu anasema kwamba Mungu alimuima haki (5)

    • Mungu wa kweli hawezi hata kidogo kutenda uovu (10)

    • Yobu anakosa ujuzi (35)

34  Kwa hiyo Elihu akaendelea kusema:   “Musikilize maneno yangu, ninyi wenye hekima;Munisikie, ninyi wenye kujua mambo mengi sana.   Kwa sababu sikio linapima manenoKama vile ulimi* unaonja chakula.   Tuchunguze kwa ajili yetu wenyewe mambo yenye kuwa sawa;Tuamue kati yetu wenyewe mambo mema.   Kwa maana Yobu amesema, ‘Niko na haki,+Lakini Mungu ameniima haki.+   Je, niseme uongo juu ya namna hukumu yangu inapaswa kuwa? Kidonda changu hakipone, hata kama sina kosa.’+   Ni mwanaume gani mwingine mwenye iko* kama Yobu,Mwenye kunywa zarau kama maji?   Yeye ni rafiki ya wakosajiNa anashirikiana na watu waovu.+   Kwa maana amesema, ‘Mwanadamu hapate faidaKwa kujaribu kumupendeza Mungu.’+ 10  Kwa hiyo munisikilize, ninyi watu wenye uelewaji:* Ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu,+Na Mweza-Yote afanye makosa!+ 11  Kwa maana atamupatia mwanadamu zawabu kulingana na matendo yake+Na ataleta juu yake matokeo ya njia zake. 12  Kwa kweli, Mungu hawezi kutenda uovu;+Mweza-Yote hawezi kupotosha haki.+ 13  Ni nani alimupatia daraka la kusimamia dunia,Na ni nani alimuweka juu ya ulimwengu wote?* 14  Kama angeelekeza uangalifu* wake juu yao,Kama angejikusanyia roho yao na pumuzi yao,+ 15  Wanadamu wote wangeangamia pamoja,Na wanadamu wangerudia katika mavumbi.+ 16  Basi kama muko na uelewaji, mukaze uangalifu juu ya jambo hili;Musikilize kwa uangalifu mambo yenye ninasema. 17  Je, mutu mwenye kuchukia haki anapaswa kuongoza,Ao je, ungemuhukumu mutu mwenye nguvu ambaye ni mwenye haki? 18  Je, unaweza kumuambia mufalme, ‘Wewe hauko wa maana,’ Ao watu wenye vyeo, ‘Ninyi muko watu waovu’?+ 19  Kuko Mutu mwenye haonyeshe wakubwa upendeleoMwenye haonyeshe upendeleo kwa matajiri na kuzarau maskini,*+Kwa maana wote hao ni kazi ya mikono yake.+ 20  Wanaweza kufa bila kutazamia,+ katikati ya usiku;+Wanatetemeka sana na kufa;Hata wenye nguvu wanaondolewa, lakini hapana kwa mikono ya mwanadamu.+ 21  Kwa maana macho ya Mungu yako juu ya njia za mwanadamu,+Na Yeye anaona hatua zake zote. 22  Hakuna giza ao kivuli kizitoMahali waovu wanaweza kujificha.+ 23  Kwa maana Mungu hajaweka wakati fulani kwa ajili ya kila mwanadamuIli aonekane mbele ya Mungu katika hukumu. 24  Anavunja-vunja wenye nguvu bila kufanya uchunguzi wowoteNa anatia wengine mahali pao.+ 25  Kwa maana anajua mambo yenye wako wanafanya;+Anawapindua wakati wa usiku, nao wanapondwa-pondwa.+ 26  Anawapiga kwa sababu ya uovu wao,Mahali kila mutu anaweza kuona,+ 27  Kwa sababu wamegeuka na kuacha kumufuata+Na wamezarau njia zake zote;+ 28  Wanafanya maskini wamulilie Mungu,Kwa hiyo anasikia kilio cha wenye hawana uwezo.+ 29  Wakati Mungu ananyamaza, ni nani anaweza kumuhukumu? Wakati anaficha uso wake, ni nani anaweza kumuona? Ikuwe kuelekea taifa ao mutu mumoja, matokeo ni sawasawa, 30  Ili mutu mwenye hamuogope Mungu* asitawale+Ao kutegea watu mitego. 31  Kwa maana, je, kuko mutu mwenye anaweza kumuambia Mungu,‘Nimepewa azabu, hata kama sikufanya kosa lolote;+ 32  Unifundishe jambo lenye sikuona;Kama nimefanya kosa lolote, sitalifanya tena’? 33  Je, Mungu akupatie zawabu kwa sababu ya maneno yako wakati unakataa hukumu yake? Unapaswa kuamua, hapana mimi. Basi uniambie mambo yenye unajua muzuri. 34  Watu wenye uelewaji* wataniambia—Kila mutu mwenye hekima mwenye ananisikia— 35  ‘Yobu anazungumuza bila ujuzi,+Na maneno yake yanakosa utambuzi.’ 36  Acha Yobu ajaribiwe* mupaka mwishoKwa sababu majibu yake ni kama ya watu waovu! 37  Anaongeza uasi juu ya zambi yake;+Anapiga mikono kwa zarau mbele yetuNa anasema maneno mengi ya kumushitaki Mungu wa kweli!”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kaakaa.” Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.
Ao “eko.”
Tnn., “moyo.”
Ao “dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”
Tnn., “moyo wake.”
Ao “watu wenye vyeo na kuzarau watu wa hali ya chini.”
Ao “muasi-imani.”
Tnn., “moyo.”
Ao pengine, “Baba yangu, acha Yobu ajaribiwe.”