Yobu 25:1-6

  • Hotuba ya tatu ya Bildadi (1-6)

    • ‘Namna gani mutu anaweza kuwa bila kosa mbele ya Mungu?’ (4)

    • Anasema kwamba uaminifu-mushikamanifu wa mwanadamu ni wa bure (5, 6)

25  Bildadi+ Mushua akajibu:   “Utawala na uwezo wenye kuogopesha ni vyake;Anaweka amani mbinguni.*   Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa? Ni nani mwenye haangaziwe na mwangaza wake?   Basi namna gani mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu,+Ao namna gani mutu mwenye alizaliwa na mwanamuke anaweza kuwa bila kosa?*+   Hata mwezi haungaeNa nyota haziko safi mbele ya macho yake,   Namna gani basi mwanadamu mwenye anaweza kufa, ambaye ni funza,*Na mwana wa binadamu, ambaye ni munyoo!”

Maelezo ya Chini

Tnn., “katika nafasi zake za juu.”
Ao “safi.”
Ao “muvunyu.”