Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAONI YA BIBLIA

Kushuka moyo

Kushuka moyo

Kushuka moyo kunamaanisha nini?

‘Nimeingiwa na wasiwasi, nimeinama kupita kiasi; nimetembea huku na huku kwa huzuni muchana kutwa.’​—Zaburi 38:6.

MAMBO AMBAYO WACHUNGUZI WANASEMA

Kila mutu anajisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo mara kwa mara, lakini ugonjwa wa kushuka moyo ni ugonjwa ambao unavuruga mutu sana na ni wenye kuendelea na unamuzuia mutu kufanya kazi zake za kila siku. Jambo ambalo tunapaswa kujua ni kwamba wachunguzi wote hawakubaliane juu ya hali ambayo ni huzuni ya “kawaida” na ile ambayo ni “kushuka moyo.” Hata hivyo, ni vizuri kusema kwamba watu fulani wanashambuliwa kabisa na mawazo yasiyofaa, na wakati fulani wanajisikia kuwa hawafae kitu na wenye makosa kupita kiasi.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Biblia inazungumuzia wanaume na wanawake wengi ambao walipambana na mawazo yasiyofaa. Kwa mufano, Hana “alikuwa na uchungu katika nafsi,” maneno ambayo yametafsiriwa “kuvunjika moyo” na “kuhangaika sana.” (1 Samweli 1:10) Wakati fulani nabii Eliya pia alikuwa na huzuni nyingi, na kwa hiyo alimuomba Mungu amuue!​—1 Wafalme 19:4.

Wakristo wa kwanza waliagizwa ‘waseme kwa kuzifariji nafsi zilizohuzunika.’ (1 Wathesalonike 5:14) Kulingana na kitabu kimoja, neno “nafsi zilizohuzunika” linaweza kumaanisha wale “ambao wanalemewa na mahangaiko ya maisha kwa muda.” Ni wazi kwamba hata wanaume na wanawake waaminifu walijisikia kuwa wenye kushuka moyo wakati fulani.

Je, kushuka moyo ni kosa la mutu ambaye anapatwa na ugonjwa huo?

“Uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja.”​—Waroma 8:22.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Bibia inafundisha kwamba ugonjwa ni matokeo ya uasi wa mwanaume na mwanamuke wa kwanza. Kwa mufano, andiko la Zaburi 51:5 linasema hivi: ‘Nilizaliwa kwa maumivu nikiwa na kosa, na mama yangu alinichukua mimba katika zambi.’ Na andiko la Waroma 5:12 linaeleza kwamba ‘kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.’ Kwa sababu tuliriti kutokamilika kutoka kwa Adamu, kila mumoja kati yetu anaweza kupatwa na ugonjwa, wa kimwili na wa kimoyoni. Kulingana na Biblia, matokeo ni kwamba “uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja.” (Waroma 8:22) Hata hivyo, Biblia inatutolea tumaini ambalo hakuna muganga anaweza kutoa, ni kusema, ahadi ya Mungu ya kuleta dunia mupya ambamo magonjwa yote yataisha, kutia ndani kushuka moyo.​—Ufunuo 21:4.

Namna gani unaweza kupambana na ugonjwa wa kushuka moyo?

“Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; naye huwaokoa wale waliopondwa roho.”​—Zaburi 34:18.

SABABU GANI NI LAZIMA UJUE JAMBO HILO?

Hauwezi kuzuia hali zote zinazoweza kukupata, na wakati fulani unaweza kupatwa na mambo mabaya. (Mhubiri 9:11, 12) Lakini, kuna mambo ambayo unaweza kufanya ili mawazo yasiyofaa yasikulemee katika maisha yako.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA

Biblia inakubali kwamba watu ambao ni wagonjwa wana lazima ya muganga. (Luka 5:31) Kwa hiyo, ikiwa unashuka moyo mara kwa mara, si vibaya kutafuta musaada kwa muganga. Biblia inakazia pia kwamba sala ni ya lazima. Kwa mufano, andiko la Zaburi 55:22 linasema hivi: ‘Mutupie Yehova muzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza. Hatamuacha kamwe mwadilifu atikisike.’ Sala si njia tu ya kukufanya ujisikie vizuri; ni mazungumuzo kabisa pamoja na Yehova Mungu, aliye “karibu na wale waliovunjika moyo.”​—Zaburi 34:18.

Unaweza pia kufaidika wakati unamufunulia rafiki yako wa nguvu sana namna unavyojisikia moyoni. (Methali 17:17) Daniela, ambaye ni Shahidi wa Yehova anasema hivi: “Muamini mwenzangu alinisadikisha kwa upole nizungumuze juu ya hali yangu ya kushuka moyo. Hata ikiwa nilikuwa ninaepuka mazungumuzo ya namna hiyo kwa miaka mingi, nilielewa baadaye kwamba hilo ndilo jambo ambalo nilihitaji kufanya kabisa. Nilishangaa na namna nilivyotulizwa kabisa kisha kueleza hali yangu.”