Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete.”​—ZABURI 139:16

Mungu Anakuelewa?

Mungu Anakuelewa?

MAMBO YENYE UUMBAJI UNATUFUNDISHA

Tufikirie uhusiano wa karibu sana wenye wanadamu wanaweza kuwa nao​—uhusiano wa mapacha wenye kufanana. Wanakuwaka na uhusiano wa karibu sana. Nancy Segal, kiongozi kwenye Twin Studies Center na mwenye kuwa pacha anasema kama mapacha fulani wanaweza kuzungumuza na kuelewana muzuri sana. Mwanamuke mumoja alieleza hivi uhusiano wake pamoja na pacha wake: “Kila mutu anajua mambo yote kuhusu mwengine.”

Ni nini inafanya waelewane kwa njia hiyo ya pekee? Uchunguzi unaonyesha kuwa, hata kama mahali kwenye mutu anaishi na namna alilelewa vinasaidia katika jambo hilo, lakini zaidi sana ni chembe za uriti zenye kufanana za mapacha wenye kufanana ndilo jambo la musingi lenye linafanya hilo litokee.

FIKIRIA JAMBO HILI: Muumbaji wa chembe hizo za ajabu, bila shaka anaelewa kwa njia ya pekee namna kila mumoja wetu ameumbwa. Kwa kweli, Daudi, muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Ulinificha katika tumbo la uzazi la mama yangu. Mifupa yangu haikufichwa mbele ya macho yako wakati nilifanywa katika siri. . . . Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete; sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chako.” (Zaburi 139:13, 15, 16) Ni Mungu tu njo anajua na anaweza kuelewa muzuri chembe zetu za uriti na pia matukio mu maisha yetu yenye yalifanya tukuwe na sifa ao tabia fulani. Uwezo wa pekee wa Mungu wa kutujua na kujua chembe zetu za uriti unatuhakikishia kuwa anatuelewa kabisa hata mu mambo madogo-madogo.

MAMBO YENYE BIBLIA INATUFUNDISHA KUHUSU UWEZO WA MUNGU WA KUJUA WANADAMU

Daudi alisali hivi: “Ee Yehova, umenichunguza kabisa, na unanijua. Unajua wakati ninakaa na wakati ninasimama. Unatambua mawazo yangu kwa mbali. Hakuna neno kwenye ulimi wangu, lakini angalia! Ee Yehova, tayari unalijua muzuri.” (Zaburi 139:1, 2, 4) Zaidi ya hilo, Yehova anajua namna tunajisikia kwa ndani na hata “anatambua kila muelekeo wa fikira.” (1 Mambo ya Nyakati 28:9; 1 Samweli 16:6, 7) Maandiko hayo yanaonyesha nini juu ya Mungu?

Hata kama wakati tunasali tunaweza kushindwa kueleza kwa sauti mawazo yetu yote na namna tunajisikia, Muumbaji wetu haone tu mambo yenye tunafanya lakini pia anaelewa sababu gani tunayafanya. Zaidi ya hilo, anajua mambo ya muzuri yenye tungependa kufanya, hata kama hali yetu inatuzuia kutimiza mambo tulipenda sana kufanya. Kwa kweli, kwa sababu upendo ni sifa ya maana sana yenye Mungu alitia katika moyo wetu, iko tayari na anatamani hata kuchunguza na kuelewa mawazo yetu yenye upendo na nia zetu.​—1 Yohana 4:7-10.

Kwa kweli, hakuna hata jambo moja lenye Mungu anashindwa kuona. Anajua mateso yetu hata wakati wengine wanaweza kukosa kuyajua ao kuyaelewa kabisa

Maandiko yanatuhakikishia

  • “Macho ya Yehova yako juu ya wenye haki, na masikio yake yanasikiliza sala yao ya kumulilia Mungu.”​—1 PETRO 3:12.

  • Mungu anaahidi hivi: “Nitakupatia ufahamu na kukufundisha katika njia yenye unapaswa kufuata. Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.”​—ZABURI 32:8.

MUNGU NI MWENYE HURUMA SANA

Kujua kama Mungu anaelewa hali yetu na namna tunajisikia, kunaweza kutusaidia kuvumilia magumu? Fikiria mambo yenye yalimufikia Anna, wa inchi ya Nigeria. Anasema hivi: “Nilijiuliza ikiwa maisha yalikuwa na maana kwa sababu nilipatwa na magumu mengi. Nilikuwa mujane mwenye kuhangaikia mutoto wangu mwanamuke, mwenye alikuwa kwenye hospitali kwa sababu ya ugonjwa wa hydrocéphalie (ugonjwa wa kuwa na umaji-maji mwingi katika ubongo). Wakati huo munganga aliniambia kama nilikuwa na kansere ya maziba. Nilipaswa kupata upasuaji, matunzo ya kemikali (chimiothérapie), na radiothérapie. Ilikuwa kabisa nguvu kuwa kwenye hospitali na wakati huohuo kuhangaikia mutoto wangu mugonjwa.”

Ni nini ilimusaidia Anna kuvumilia? “Nilifikiri sana juu ya maandiko kama vile Wafilipi 4:6, 7, yenye kusema kama ‘amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili.’ Kila mara wakati nilikumbuka andiko hilo, nilijisikia kuwa karibu na Yehova, nikijua kama ananielewa muzuri zaidi kuliko mimi mwenyewe. Ndugu na dada zangu wa kiroho katika kutaniko la Kikristo walinitia pia moyo.

“Hata kama ninaendelea kupambana na afya yangu, hali yangu na ya mutoto wangu mwanamuke imekuwa muzuri kuliko zamani. Kwa sababu Yehova iko upande wetu, tumejifunza kuepuka mawazo yenye hayafae wakati tunapambana na magumu. Yakobo 5:11 inatuhakikishia hivi: ‘Tunaona wale wenye wamevumilia kuwa wenye furaha. Mumesikia juu ya uvumilivu wa Yobu na mumeona matokeo yenye Yehova alileta, kwamba Yehova ni mwenye upendo mwingi sana [ao, “mwenye huruma sana,” maelezo ya chini] na mwenye rehema.’” Yehova alielewa muzuri hali ya Yobu, na sisi pia tunaweza kuwa hakika kama anaelewa magumu yoyote yenye tunapambana nayo.