Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Nani Anatuletea Mateso?

Ni Nani Anatuletea Mateso?

Ikiwa haiko Mungu ndiye anatuletea mateso, ni nani anafanya watu wengi waishi katika njaa kubwa, umaskini wenye hauishe, vita kali, magonjwa hatari, na misiba ya asili? Neno la Mungu, Biblia, linaonyesha sababu tatu kubwa zenye zinafanya watu wateseke:

  1. Uchoyo, Pupa, na Chuki. “Mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.” (Muhubiri 8:9) Mara nyingi watu wanateseka kwa sababu ya watu wenye hawakamilike, wachoyo, ao watu wakali.

  2. Wakati na Matukio Yenye Hayatazamiwe. Mara nyingi watu wanateseka “kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe yanafikia wote.” (Muhubiri 9:11) Ni kusema, watu wako pa nafasi ya mubaya kwa wakati mubaya, aksidenti zinatokea, ao watu hawako waangalifu ao wanafanya makosa.

  3. Mutawala Muovu wa Ulimwengu. Biblia inaonyesha waziwazi sababu kubwa yenye inafanya wanadamu wateseke. Inasema hivi: “Ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yohana 5:19) Ule “muovu” ni Shetani Ibilisi, kiumbe wa roho mwenye nguvu ambaye zamani alikuwa malaika wa Mungu lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Viumbe wengine walijiunga na Shetani na kumuasi Mungu ili kutimiza tamaa zao za uchoyo, na kwa hiyo wakajifanya kuwa pepo wachafu. (Mwanzo 6:1-5) Tangu uasi wao, Shetani na pepo wake wachafu wamechochea kwa njia mubaya sana mambo ya ulimwengu. Hilo limeonekana zaidi sana leo. Leo, Ibilisi iko na kasirani kali na “anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu,” na hilo limeleta “ole wa dunia.” (Ufunuo 12:9, 12) Kwa kweli, Shetani ni mutawala mukali sana. Anafurahi sana wakati watu wako wanateseka. Ni Shetani ndiye anafanya watu wateseke, haiko Mungu.

FIKIRIA JAMBO HILI: Ni mutu tu mwenye hana huruma na mubaya sana ndiye anaweza kufanya watu wenye hawana kosa wateseke. Lakini kuhusu Mungu, Biblia inasema hivi: “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Kwa sababu yeye ni upendo, “ni jambo lenye haliwezi kuwaziwa kwamba Mungu wa kweli atende uovu, na Mweza-Yote afanye makosa!”​—Yobu 34:10.

Hata hivyo, pengine unaweza kujiuliza, ‘Ni mupaka wakati gani Mungu Mweza-Yote ataacha Shetani aendelee kutawala kwa ukali?’ Kama vile tumekwisha kuona, Mungu anachukia sana mambo maovu na mateso yetu yanamuumiza sana. Zaidi ya hilo, Neno lake linatutia moyo hivi: “Mumutupie mahangaiko yenu yote, kwa sababu yeye anawahangaikia ninyi.” (1 Petro 5:7) Mungu anatupenda na iko na nguvu ya kuondoa mateso yote na ukosefu wa haki, kama vile tutaona katika habari yenye kufuata. *

^ fu. 7 Ili kupata habari zaidi kuhusu sababu gani Mungu ameruhusu mateso, ona sura ya 11 ya Kitabu Biblia Inatufundisha Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza kukichukua bila kulipa kwenye www.mt711.com.