Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Uko na Ugonjwa Hatari

Wakati Uko na Ugonjwa Hatari

“Wakati niliambiwa kama niko na ugonjwa wa kansere kwenye pafu (poumon) na kwenye utumbo-tumbo pana, niliwaza kama nimepewa hukumu ya kifo. Lakini, wakati nilienda ku nyumba kisha kuonana na munganga, niliwaza, ‘Sawa, sikutumainia kama mambo itakuwa vile, lakini ninapaswa kutafuta namna ya kupambana na hii hali.’”​—Linda, iko na miaka 71.

“Niko na ugonjwa wenye kuumiza sana wenye kushambulia mishipa yenye kuwa kwenye upande wa kushoto wa sura yangu. Wakati fulani, maumivu makali ilinifanya nikuwe mwenye kushuka moyo. Mara mingi, nilijisikia peke yangu na niliwaza hata kujiua.”​—Elise, iko na miaka 49.

IKIWA wewe ao mupendwa wako ameambiwa kama iko na ugonjwa wenye unaweza kuleta kifo, unajua namna jambo hilo linaweza kuvunja moyo. Zaidi ya ugonjwa wenyewe, unapaswa kupambana na mahangaiko ya akili kwa sababu ya hali hiyo. Programu ya kuonana na munganga yenye kuhangaisha, magumu ya kupata ao kulipia matunzo, ao matokeo ya mubaya yenye inaweza kuletwa na dawa yenye unatumia, vinaweza kukuongezea woga na wasiwasi. Mahangaiko ya akili yenye kuhusiana na ugonjwa hatari inaweza kuchokesha sana.

Ni wapi tunaweza kupata musaada? Watu wengi wametambua kama wanapata kitulizo kikubwa zaidi kwa kusali kwa Mungu na kusoma maandiko yenye kutuliza yenye kupatikana katika Biblia. Musaada mwingine tunaweza kuupata kupitia watu wa familia na marafiki wenye upendo na wenye wanaweza kututegemeza.

MAMBO YENYE ILISAIDIA WENGINE WAVUMILIE

Robert mwenye kuwa na miaka 58, alishauri hivi: “Ukuwe na imani katika Mungu na atakusaidia kuvumilia ugonjwa wako. Sali kwa Yehova. Umuambie namna unajisikia. Umuombe roho takatifu. Umuombe akusaidie ukuwe na mawazo ya muzuri na ukuwe mwenye kutia moyo watu wa familia na uvumilie ugonjwa wako ukiwa mwenye kutulia.

“Wakati watu wa familia yako wako pale kwa ajili yako na wakati wanakutia moyo, ile inasaidiaka sana. Kila siku, mutu mumoja ao watu wawili wa familia yangu wananiita ku telefone na kuniuliza, ‘Unaendelea je?’ Marafiki wangu wenye kuishi sehemu mbalimbali wananitia moyo. Wananifanya nijisikie muzuri zaidi, na ile inanisaidia nivumilie.”

Ikiwa unatembelea rafiki yako mwenye ni mugonjwa, fikiria jambo lenye Linda anasema: “Bila shaka mugonjwa anapendaka kuishi maisha ya kawaida kadiri inawezekana na hawezi kupenda kila mara kuzungumuzia magonjwa yake. Kwa hiyo, uzungumuzie mambo yenye unazoea kuzungumuzia.”

Kupitia nguvu yenye kutoka kwa Mungu na kitulizo kutoka katika Maandiko, na pia kupitia musaada wenye upendo wa watu wa familia na marafiki, tunaweza kuwa hakika kama maisha ni ya maana, hata wakati tunapambana na ugonjwa hatari.