Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakati Unajisikia Kuwa Haupendi Tena Kuishi

Wakati Unajisikia Kuwa Haupendi Tena Kuishi

Adriana mwenye kuishi Brazili, anasema hivi: “Mahangaiko yangu makali iliendelea kunitesa sana. Kwa hiyo, niliona kama ingekua muzuri zaidi nikufe.”

JE, UMEKWISHA kujisikia mubaya sana hivi kwamba haukupenda tena kuishi? Kama ni vile, unaweza kuelewa namna Adriana alijisikia. Aliteswa na mahangaiko makali na alijisikia kuwa mwenye huzuni na bila tumaini. Adriana alivumbuliwa na ugonjwa wenye kufanya mutu akuwe mwenye huzuni kila wakati.

Fikiria pia mwanaume mumoja wa Japani mwenye kuitwa Kaoru, mwenye alichunga wazazi wake wagonjwa-wagonjwa na wenye kuzeeka. Anasema hivi: “Wakati huo, nilihangaishwa na mukazo mukali ku kazi. Kisha wakati fulani, nilipoteza hamu yangu ya kula, na sikuweza kulala muzuri. Nilianza kuwaza kuwa matatizo yangu ingeisha ikiwa ningekufa.”

Ojebode, mwanaume mumoja wa Nigeria anasema hivi: “Kila wakati nilikuwa na huzuni hivi kwamba nilifikia kulia; kwa hiyo, nilitafuta njia ya kumaliza uzima wangu.” Jambo lenye kufurahisha ni kuwa, Ojebode, Kaoru, na Adriana hawakujiua. Lakini kila mwaka mamia ya maelfu ya watu wanajiua.

KWENYE TUNAWEZA KUPATA MUSAADA

Watu wengi wenye wanajiua ni wanaume, na wengi kati yao walisikia haya sana ya kuomba musaada. Yesu alisema kama wagonjwa wako na lazima ya munganga. (Luka 5:31) Kwa hiyo, ikiwa uko na mawazo ya vile, tafazali usisikie haya kuomba musaada. Watu wengi wenye kushuka moyo wameona kuwa matunzo ya kinganga inaweza kuwasaidia kuvumilia. Ojebode, Kaoru, na Adriana wote walipata musaada kutoka kwa wanganga na sasa wanapambana muzuri zaidi na hali yao.

Wanganga wengi wanaweza kutumia dawa ao kuzungumuza na mugonjwa kuhusu namna ya kubadilisha mawazo na tabia zake, ao wanaweza kutumia njia zote mbili ili kutunza hali yake ya kushuka moyo. Wale wenye wanateseka wako pia na lazima ya kuona kuwa watu wa familia yao na marafiki wanawaelewa, wanawatendea kwa uvumilivu, wanawahangaikia na kuwategemeza. Rafiki wa muzuri zaidi mwenye kila mutu anaweza kupata ni Yehova Mungu, mwenye anatoa musaada wa muzuri sana kupitia Neno lake Biblia.

JE, MAMBO YENYE KUUMIZA ITAISHA KABISA?

Mara mingi wale wenye wameshuka moyo wanakuwaka na lazima ya matunzo yenye kuendelea na wanapaswa kujifunza namna ya kuvumilia kwa kufanya mabadiliko katika namna yao ya kuishi. Lakini ikiwa unapambana na hali ya kushuka moyo, unaweza kungojea kwa hamu wakati wenye kuja wenye furaha kama vile Ojebode anafanya. Anasema hivi: “Ninangojea kwa hamu kuona utimizo wa andiko la Isaya 33:24 lenye linatabiri wakati wenye katika dunia hakuna mutu yeyote mwenye atasema ‘Niko mugonjwa.’” Kama vile Ojebode, upate faraja katika ahadi ya Mungu ya “dunia mupya,” mwenye hamutakuwa tena “maumivu.” (Ufunuo 21:1, 4) Ile ahadi inatia ndani kumaliza maumivu yote ya kiakili na ya moyoni. Hisia zako zote zenye kuumiza zitaisha milele. Kwa kweli, mambo yote yenye kuumiza “hayatakumbukwa, wala hayataingia katika moyo [wako].”​—Isaya 65:17.